Chozi la Heri By Assumpta K. Matei

by sava in Text book centre buy now Publishered by: sava

Chozi la Heri By Assumpta K. Matei Details


Fasihi Tambuzi ya Kiafrika (FATAKI)

Chozi la Heri

"Mungu wangu! Huyu si ndugu yangu Mwaliko?" Umu alisema kimyakimya. Dick naye alikuwa kaghumiwa, hajui la kusema. Anamtazama mnuna wake kana kwamba ni Mr Super Man katika sinema pendwa za kijasiri. Wote wawili walitazarnana, kila mmoja akiapa moyoni kuwa amewahi kumwona kiumbe huyu mahali, lakini hakuna aliyethubutu kunena...

Tamaa ya kumiliki nyenzo za kujiinua kiuchumi na kisiasa, kama inavyodhihirika katika riwaya hii, inasambaratisha asasi za kijamii, pamoja na miundomsingi ya mshikamano wa kijamii. Maazimio yasiyofikiwa yanazua hali ya kuvunjikiwa—kihoro hasa. Lakini baada ya kiza kizito huja mawio ya uzawa wa jamii mpya yenye matumaini.

Assumpta K. Matei ni mtafiti na mwalimu mwenye tajiriba papa katika ufundishaji wa lugha na fasihi ya Kiswahili katika shule za upili na vyuo vikuu. Kati ya taasisi alizowahi kufundisha ni Kenya High School na Catholic University of Eastern Africa. Ameshiriki katika majopo mbalimbali ya ukuzaji, utekelezaji na tathmini ya mitaala. 

ISBN: 9789966068439 SKU: 2010129000207